POLITICAL

Sema Kenya - Jukwaa la Wakenya

 Sema Kenya…jukwaa la WaKenya wote, jiunge na mjadala wa kitaifa.
Sema Kenya ni kipindi cha mjadala, cha muda wa saa moja, ambacho hupeperushwa kupitia redio, televisheni na kwenye tovuti.
Kipindi hiki kinazuru maeneo tofauti ya nchi, huku Wakenya wakijiandaa kufanya uchaguzi mkuu mwezi Machi mwaka ujao. Lengo ni kuwapa wananchi fursa ya kuelezea hoja zao, kupata taarifa na kushiriki katika mjadala wa kitaifa.
Tangu kilipozinduliwa mwezi Oktoba, Kipindi cha Sema Kenya kimefaulu kuandaa mijadala mikali iliojumuisha wananchi ikiangazia masuala ya usalama, mihadarati, ukabila, ugatuzi, ugavi wa ardhi na marekebisho ya sheria za ugavi wa ardhi.
Mada za kila kipindi huamuliwa na washiriki.
Watu wanaweza kushiriki katika mazungumzo haya ya kitaifa kupitia tovuti ya BBC, mitandao ya kijamii ya Facebook na Twitter. Aidha njia nyingine Sema Kenya inawafikia wananchi ni kupitia mashirika ya kijamii ambayo kipindi hiki kinashirikiana nao.
Mtindo wa Sema Kenya:
• Lugha: Sema Kenya inaendeshwa kwa lugha ya Kiswahili.
• Utafiti: Sema Kenya inategemea utafiti wa kina kufanikisha makala haya.
• Wanaoshiriki: Kinahusisha watu wa tabaka mbalimbali; vijana kwa wazee, wanawake na wawakilishi wa vikundi maalum.
• Huwaleta pamoja wananchi na viongozi wao: Wananchi wa kawaida na jamii zilizotengwa wanapata fursa ya kuwahoji viongozi wao.
• Mada ya mjadala huamuliwa na washiriki katika kipindi hiki.
• Haibagui, haipendelei na inashirikisha kila moja kupitia redio, televisheni na kwenye tovuti.
• Mjadala huendelea kwenye mtandao wakati kipindi kikiwa hewani hata baada ya kutia tamati kwenye redio na televisheni.
Tazama, Sikiliza na ushiriki kwa Sema Kenya
Televisheni: KTN, kila Jumapili saa 6 jioni.
Redio: Idhaa ya Dunia ya BBC (Nairobi 93.9FM, Mombasa 88.1FM) na kupitia kituo cha Pamoja FM kila Jumapili saa saba alasiri.
Mtandao: bbcswahili.com/semakenya
Facebook: BBCSemaKenya
Twitter: @ bbcsemakenya
Sema Kenya ... Jukwaa la Wakenya, jiunge na mazungumzo ya kitaifa.

 

Dennis Rodman asks Kim Jong Un to let U.S. citizen go

By Holly Yan and Jethro Mullen, CNN
May 8, 2013 -- Updated 0935 GMT (1735 HKT)
Dennis Rodman attended a basketball game with Kim Jong-un during his visit to North Korea in February.
Dennis Rodman attended a basketball game with Kim Jong-un during his visit to North Korea in February.

STORY HIGHLIGHTS
  • Dennis Rodman: "Do me a solid and cut Kenneth Bae loose"
  • Bae was sentenced to 15 years of hard labor in North Korea for unspecified "hostile acts"
  • His sister says Bae owns a tour company and is not a spy
  • Rodman has called North Korean ruler Kim Jong Un a "friend for life"
(CNN) -- If any American has the power of persuasion over North Korea's defiant young ruler, it might be eccentric ex-basketball star Dennis Rodman.
So when Rodman digitally called for Kim Jong Un to release U.S. citizen Kenneth Bae, he may have a shot at a response.
"I'm calling on the Supreme Leader of North Korea or as I call him "Kim", to do me a solid and cut Kenneth Bae loose," Rodman tweeted.
Bae was sentenced to 15 years of hard labor last month after he was convicted of unspecified "hostile acts" against North Korea. The country's state-run Korean Central News Agency said the Korean-American was arrested November 3 after arriving as a tourist in Rason City, a northeastern port near the Chinese border.

Americans detained abroad Americans detained abroad

Sister baffled by North Korea punishment

Rodman reveals North Korea secrets

Rodman: I'm going back to North Korea
"He has never had any evil intentions against North Korea, or any other country for that matter," Chung said.
She said her brother owns a tour company and was in North Korea for work.
"He didn't have any problems going there last time, last year five times, so he didn't have any reason to suspect that there would be any trouble this time around," she said.
U.S. officials have struggled to establish how exactly Bae fell afoul of North Korean authorities. The North Korean statement on his conviction provided no details of the allegations against him.
"This was somebody who was a tour operator, who has been there in the past and has a visa to go to the North," a senior U.S. official told CNN on Monday, speaking on condition of anonymity because of the diplomatic sensitivity of the issue.
But NK News, a U.S.-based website that focuses on North Korea, suggests Bae has served as a missionary trying to convert North Koreans.
"I knew that Jesus wanted me to be a 'channel' to the North," Bae told a Korean congregation at a St. Louis church in 2011, NK News reported. "This year, I'm working at taking several short term missionary teams into North Korea."
Bae's sentencing came after weeks of intense rhetoric from North Korea, which conducted its third nuclear test in February and launched a satellite into orbit atop a long-range rocket in December.
Washington responded by deploying additional missile interceptors on the West Coast, dispatching a missile defense system to the Pacific territory of Guam and bolstering annual U.S.-South Korean military exercises with overflights by nuclear-capable B-2 and B-52 bombers.
Rodman, the heavily pierced NBA Hall of Famer, made headlines when he befriended North Korea's supreme leader during a visit in February.
"You have a friend for life," Rodman told Kim after the two men sat next to each other watching an unusual basketball exhibition in Pyongyang.
But Rodman said he is not an official diplomat between the United States and North Korea.
"I'm not a politician," he tweeted. "Kim Jung Un & North Korean people are basketball fans. I love everyone. Period. End of story."





MORSI AKAIDI MAKATAA YA JESHI
Rais wa Misri Mohammed Morsi
Rais wa Misri Mohammed Morsi amesisitiza kwamba yeye ndiye kiongozi halali wa taifa huku maandamano kati ya wapinzani na wafuasi wake yakisababisha vifo zaidi.
Kwenye hotuba aliyotoa kwa taifa usiku wa kuamkia leo, Mosri alipinga makataa ya jeshi kutatua mgogoro wa sasa ifikapo Jumanne. Kiongozi huyo amesema hataamrishwa na yeyote na kuwasihi waandamanaji kuweka utulivu.
Hata hivyo watu 16 walikufa katika moja wapo ya maandamano ya wafuasi wa Morsi. Awali jeshi lilitoa mpango wa kurejesha taifa katika uthabiti.
Stakabathi iliyopatikana na BBC inasema jeshi linapanga kuvunja katiba, kuweka machakato wa uchaguzi mkuu, na kuvunja bunge.
Hapo Jumatatu Jeshi lilisema huenda likaingilia kati ikiwa hali haitabadilika. Morsi na wanasiasa walipewa saa 48 kuafikiana.








 

Rais Barack Obama awasili Tanzania

 
Na; Raymond Claud
Rais Barack Obama wakati wa ziara yake Afrika Kusini
Rais wa Marekani Barack Obama, amewasili nchini Tanzania katika mkondo wake wa mwisho wa ziara yake barani Afrika.
Ziara ya Obama inasemekana kulenga kuimarisha uhusiano wa kibiashara na Afrika huku kukiwa na wasiwasi kuwa Marekani inaachwa nyuma na China katika uhusiano wao na Afrika.
Obama amewasili Tanzania baada ya ziara yake ya Afrika Kusini ambako rais mstaafu Nelson Mandela anaugua.
Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete na familia yake pamoja na maafisa wake wa serikali na wacheza densi za kitamaduni walimkaribisha Obama na familia yake mjini Dar es Salaam.
Baadhi ya wananchi wa Tanzania kupitia mitandao ya kijamii wamekosoa ziara ya Obama katika nchi yao, wakisema kuwa ziara yake imeathiri shughuli za maisha yao ya kila siku.
Obama alitembelea Senegal kabla ya kupitia Afrika Kusini na kisha Tanzania ambako ziara yake ya Afrika inaishia kabla ya kurejea Marekani.
Obama ameambatana mamia ya wafanyabiashara na swala la uchumi linatarajiwa kupewa kipamboele kwenye ajenda.
Aidha Obama atatembelea kiwanda cha kuzalisha umeme kinachomilikiwa na Marekani kufuatia tangazo lake mwishoni mwa wiki wa mpango wa mabilioni ya dola kufadhili mradi wa uzalishaji wa kawi.
Mpango huo wa miaka mitano, unatarajiwa kuwezesha nchi nyingi Afrika kuweza kupata kawi kwa ushrikiano na nchi zingine za Afrika na sekta binafsi.
Wakati wa ziara yake, nchini Afrika Kusini, kiongozi huyo wa Marekani hakumtembelea Mandela ambaye anasalia kuwa mahututi hospitalini akiigua maradhi ya mapafu.
Duru zinasema kuwa barabara zimefungwa na usalama kudhibitiwa vilivyo, mjini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment